Vidokezo hivi 10 huwasaidia wasichana…

Kuonyesha uwezo wao kwa kuongoza

1. Ukiwa darasani simama na uongee

Wewe nyoosha tu mkono hata kama hauna uhakika na majibu yako,usijisumbue kusahihisha kichwani kile unachotaka kukisema na waala usiwaze ukikosea itakuwaje,kuongea haimanishi kuwa lazima uwe na jibu sahihi,Inakupa uzoefu wa kuwa kusimama wewe kama wewe ili kujadiliana,kushindana mawazo,uzoefu ambao utakusaidia katika sehemu mbalimbali kwenye maisha yako

**Acha kuwa unaomba samahani kabla ya kuzungumza

Maranyingi wasichana hutoa maoni yako huku wakiomba kwanza samahani (“Samahan Sina uhakika kama hiki ni sahihi lakini…”.) Angalia sana nyakati ambazo unajishusha sanaa unapokuwa ukisema kitu darasani,Mfano unawambia “unafikiria kitu” huku unachezea kalamu,unawauliza kama ulicho sema ni “sahihi ama sio sahihi”au unaongea kwa sauti ya chini ambayo hata hawakusikii.

Jipe changamoto

Wakati tunapokuwa tunaogopa kufeli au kukosolewa,huwa tunaangalia uwezo tuloonao katika kuikabili hali na kushinda.Lakini tunapokuwa tunakabili hali kama hizi kwa kwa kujikuta eti unaogopa hatari zinazoweza kukukabili inamaanisha hutawahi kamwe kuwa na msukumo kupambana na vikwazo na kuuthibitishia ulimwengu na wewe pia ya kuwa una ujasiri wa kutosha katika kujaribu mambo. Jiunge kwenye mchezo ambao hujawahi kuucheza,Jiunge na kozi ambayo hakuna mtu ambaye angewaza uisome, Jifunze namna ya kutumia kompyuta,Au hata jifyatue tu akili ukamuongeleshe mtu usiemjua na ujitambulishe kwake.

4. Omba Usaidizi

Watu waliofanikiwa zaidi hawafaulu kivyao. Badala yake, wanawapata washauri maishani: watu wenye uzoefu, wenye hekima wanaojua mengi na kuwasaidia. Usiogope kuwauliza walimu, wakufunzi, au watu wengine wazima unaotamani kuzungumza nao kuhusu unachokipenda. Waulize kile ambacho walitamani kujua walipokuwa na umri wako. Nani anayejua, huenda siku moja wanaweza hata kukusaidia kufanya ndoto zako kutimia!

5. Usifanye Kile Anachokifanya Kila Mtu

Mwanachama wa mradi wa kikundi asipochangia vyema (au kabisa), ni rahisi kulifanya mwenyewe – na unyamaze. Kuchukua mamlaka kunaweza kukupa udhibiti kwa muda, lakini kunaweza pia kukufanya kuwa na hasira, kufanya kazi nyingi, na kutoshukuriwa. Tatua tatizo moja kwa moja kwa kumwuliza mwenzako wa darasani wakati anaodhani kuwa atakamilisha kazi zake. Usipopata jibu la wazi, sema unachokihitaji moja kwa moja, au mwombe mwalimu akusaidie.

6. Zungumza katika Urafiki

Huenda sote tumesengenya kwa namna moja au nyingine, lakini ukizungumza kila mara kuhusu marafiki zako badala ya kuzungumza nao , unakosa fursa ya kujifunza kuzungumza na watu muhimu zaidi. Kuwa na uwezo wa kumwambia mtu namna unavyohisi kutakusaidia katika kila sehemu ya maisha yako, haijalishi namna unavyochagua kukumbatia hatari. Na huenda ukataka kuepuka kutegemea kutuma ujumbe au mitandao ya jamii kusema mambo mazito. Inarahisisha mawasiliano muda huu, lakini utakuwa katika hatari ya kulipa baadaye kwa kutozungumza ana kwa ana sasa. Kutenda moja kwa moja kunatisha, lakini kufanye kwa uangalifu na utapata heshima na uaminifu wa wale walio karibu nawe.

7. Iamini Sauti Yako ya Ndani

Sote tuna sauti inayocheza vichwani mwetu. Huenda ikasema vitu vidogo kama “Ninatamani kengele ilie” au vitu vikubwa kama “Ninatamani rafiki yangu akome kuniuliza kuhusu alama zangu.” Sauti ni ujasiri wako. Inakuambia unachokifikiria, kuhitaji na kutaka. Ni rahisi kuacha kusikiliza sauti hiyo ukiwa na wasiwasi kuhusu kile watu wanachoweza kufikiria. Endelea kuambatana nayo kadri uwezavyo. Ndiyo dira yako ya ndani. Kama huwezi kushiriki sauti hiyo sasa, weka jarida unapoweza kushiriki – na uendelee kuwatafuta watu wanaotaka kuisikiliza.

8. Ibadilishe Dunia

Si lazima uongoze dunia ndipo uibadilishe. Ni nini kinachokuangazia ndani? Ni nini kinachokufanya kuhisi kukasirishwa? Jiunge na klabu au anzisha shirika la jamii. Huenda hata KUPIGIWA kura kuwa rais wa darasa. Kufanya kampeni kunakupa mazoezi ya ajabu ya kuzungumza na kujitangaza kama kiongozi. Chochote unachoamua, kumbuka: sauti yako si kama ya mtu mwingine, lakini hatutaisikia usipoitumia.

9. Kumbuka: Haiwi Rahisi Kila Mara Kuzungumza, lakini Ni Heri

Unakua katika ulimwengu ambao bado umechanganyikiwa kuhusu namna unavyotaka wasichana wawe wenye nguvu. Wasichana wanahitajika kuwa jasiri lakini waungwana, wenye kutaka makuu lakini si wabinafsi, wenye ufanisi lakini si wenye majivuno. Sheria zinaweza kuchanganya na zisizo za haki – kumaanisha si kila mtu atakayefurahia ukizungumza. Kwanza, haijalishi ni vipi unavyosema kitu vyema, kunaweza kuwepo mtu anayefikiria wewe ni mchoyo. Iamini sauti yako hata kama inaonekana kuwa dunia haitaki, na uwe karibu na marafiki na wanafamilia wanaokuunga mkono. 10. Fanya mazoezi! Umekua kwa kufanya mazoezi ya vitu kama kazi ya shuleni, michezo, na muziki. Lakini hakuna mtu anayekuambia ufanye mazoezi ya kuzungumza, kuchukua tahadhari, au kusema unachokihitaji. Hicho kina nini? Hakuna chochote duniani kisichohitaji mazoezi, hata kuzungumza. Tia juhudia! Inaweza kutisha mara ya kwanza, lakini inakuwa rahisi baadaye.

Vidokezo kwa udhamini wa http://banbossy.com

Share your feedback