Mwalimu wangu, mwanatimu mwenzangu

Vidokezo vya kukusaidia kujiunga na timu

“Somo linakanganya sana!”

“Je, ninawezaje kupata alama za juu shuleni?”

“Mitihani inanitia usongo.”

Maisha ya shule yanafurahisha. Lakini wakati mwingine, kushughulikia masuala mengine, shughuli za burudani, vile vile mambo yetu binafsi, unaweza kuhisi kana kwamba hayo ni mambo mengi usiyoweza kuyashughulikia. Lakini lingekuwa jambo zuri ikiwa tungempata mtu wa kutusaidia wakati huu wa kuchanganyikiwa. Mwanatimu wa aina yoyote ambaye atatutia moyo na kutupa mwongozo wakati tunapouhitaji? Mmm, kwa bahati nzuri tuna mtu kama huyo! Na amini usiamini,, mwanatimu huyo amekuwa mbele yetu muda huu wote -- walimu wetu!

Ingawa wengi wetu sisi wasichana hatuwezi kuthubutu kuwaendea walimu wetu kwa sababu ya dhana tuliyonayo kwamba wanatisha na wanaweza kutunyanyasa, sharti tukumbuke kwamba walimu wapo kwa ajili ya kutusaidia kufanikiwa na kupata alama nzuri shuleni. Utashangaa jinsi uhusiano mzuri kati ya mshauri na mwanafunzi unaweza kusaidia kwa njia kuu si tu katika masomo yetu, lakini vile vile maisha yetu ya binafsi. Hapa kuna vidokezo vya kutusaidia ili tuweze kufaidika sana kutoka kwa walimu wetu.

Twisheni –Hata ikiwa darasa limeisha, bado tunaweza kuwaomba walimu wetu watusaidie kimasomo. Tukiwa na vipindi vya mafundisho baada ya muda wa shule kuisha au kupewa kazi za ziada za nyumbani, tutaweza kuelewa masomo vizuri na kujiandaa kwa utulivu kwa ajili ya mitihani inayokuja.

Ushauri – Usiogope kuwaendea walimu wetu na kuwauliza maswali. Ushauri hutupa fursa ya kurekebisha yale ambayo huenda tumeyakosa katika kipindi cha masomo. Hii pia ni fursa kwetu ya kuweza kujifunza mambo ya ziada kupita yale yaliyofundishwa shuleni.

Uraibu Binafsi – Msaada tunaoweza kupewa na walimu wetu hauishii tu katika masomo yetu. Pia wanaweza kutusaidia katika uraibu wetu binafsi kama vile starehe, au hata kuchagua taalamu yetu ya mbeleni. Walimu ni watu wa kuheshimika ambao tunaweza kuwaamini watusaidie kihisia na kiakili kama tunavyohitaji.

Kwa hiyo wana Springsters, kumbuka, ikiwa unahitaji msaada wa ziada katika masuala ya shule au hata mambo binafsi, yupo mwanatimu ambaye yuko tayari kutusaidia – walimu wetu! Tunachopaswa kufanya ni kuomba tu!

Je una mtu wa kuongea nae unapohitaji msaada katika masomo yako au hata mambo yako binafsi? tuambie hapo chini kwenye sehemu ya maoni.

Share your feedback