Jinsi ya Kuomba Msaada

Vidokezo 5 kutoka Tujibebe!

Mawazo yako (2)

Kuna wakati unaweza kuzidiwa na maisha kutokana na majukumu na ndoto ulizonazo. iwe kujiandaa na mitihani, kujaribu kuanzisha biashara ndogo au kufikiria maisha ya kazi za baadaye, hakika maisha yana mambo mengi ya kufikiria!

Kuna nyakati tunaomba msaada toka kwa wazazi au walezi wetu lakini tunaogopa majibu yao au ushauri wanaotupa na kusababisha tuogope kuanzisha mazungumzo. Hili likitokea tunapoteza fursa ya kupata msaada. Kuomba ushauri kwa wazazi au walezi wetu hutusaidia kuwa katika mwelekeo sahihi. Tujibebe inakupa vidokezo 5 vitakavyokusaidia kuanzisha mazungumzo na wazazi au walezi ikiwa unapata tabu kufanya hivyo!

1. Tafuta muda mzuri na tulivu wa kuongea
Inaweza kuwa ngumu kupata usikivu wa mtu kama utachagua wakati ambao anashughuli, majukumu au mambo mengi. tunapaswa kujaribu kupanga wakati ambao watakuwa na uhuru wa kuongea na kutusikiliza kwa umakini. Panga muda mapema, ni vizuri zaidi wakiwa wamepumzika, hivyo wataweza kusikiliza kwa umakini, wajulishe kuwa unajambo la muhimu la kuongea nao.

2. Zungumza waziwazi na kwa ujasiri
Kufanya mazoezi ya lile tunalotaka kuongea, kwa kuongea kwa nguvu na kujiamini au kuandika huwa inasaidia kwa ajili ya maandalizi. Tukiongea kwa ujasiri inaonyesha kuwa tuko makini na inaweza kuwa rahisi kwa mtu mwingine kuelewa kuwa tumedhamiria na tunatumaini watakuwa na utayari wa kutusikiliza na kujifunza.

3. Tengeneza mpango
Tukifikiria kuhusu aina ya maswali tunayoweza kuulizwa, tunaweza kutayarisha majibu kwa ufasaha na kuwasaidia kuelewa mtazamo wetu. Jaribu kufikiria juu ya kile wanachoweza kusema au kuuliza na jitayarishe jinsi ya kujibu maswali. Maandalizi husaidia mambo kwenda vizuri zaidi.

4. Angalia upande wao Hii inaweza kuwa ngumu sana lakini kwa kufanya hivyo, tunaweza kujifunza kuona matatizo yetu katika mtazamo wa walezi au wazazi. Wakati mwingine wanaweza kutupa ushauri ambao hatutaki kusikia lakini tunapaswa kujaribu kusikiliza na kuelewa mtazamo wao.

5. Lazima uwe na mpango mbadala.
Kama hawatatupa majibu mazuri, hatupaswi kushindana nao. Acha wao waseme, na uwaambie kwamba unaelewa mtazamo wao na ungependa kuwa na nafasi ya kujieleza zaidi. Jaribu kutafuta maelewano yatakayo wafanya wote mfurahi. Kama unaona sio wakati sahihi unaweza kujaribu tena baadaye.

Share your feedback

Mawazo yako

Mamb vp wapendwa asuby njema

Machi 20, 2022, 8:25 p.m

Latest Reply

Mko pw